Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wakazi Japan wajiandaa dhidi ya shambulio la Korea Kaskazini
Wakaazi wa mji mmoja ulioko kaskazini magharibi mwa pwani ya Japan, wameendesha zoezi la kukabliana na hali ya hatari na kujiandaa kwa shambulizi la aina yoyote, ikiwa Korea Kaskazini itaamua kuwashambulia kwa makombora.
Zaidi ya watu 100 walihusika katika zoezi hilo lililofanyikia maeneo ya Oga huko Akita, kwa kukimbilia hifadhi shuleni na katika vituo vya kuwahudumia jamii.
Walipokea tahadhari kupitia simu zao za mkononi.
Mapema mwezi huu, makombora matatu ya Korea Kaskazini yaliangushwa katika maeneo ya maji yaliyoko pwani ya Japan.