Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Meli ya Marekani yaionya ile ya Iran
Maafisa wa ulinzi wa Marekani wamesema kuwa meli ya kivita ya Marekani imefyatulia risasi kadhaa meli ya Iran katika Ghuba.
Meli hiyo ijulikanayo kama The USS Thunderbolt ilifyatulia meli ya Iran baada ya meli hiyo kukiuka mawasiliano ya radio.
Meli hiyo ya Iran inayosemekana kusimamiwa na kikosi maalumu cha kijeshi nchini - Iranian Revolutionary Guard - ilikuwa ikienda kwa kasi na ikafika mita 50 karibu na meli hiyo ya Marekani.
Hakuna habari zo zote zilizotolewa na Iran.