Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Majeshi ya Cameroon tuhumani
Ripoti mpya iliyotolewa na Shirika la Haki za Binadamu la Amnesty International limedai kwamba majeshi ya Ulinzi ya Cameroon yamewatesa na kuwaua watuhumiwa kadhaa wanachama wa kundi lenye siasa kali la Boko Haramu.
Ripoti hiyo imesema miongoni mwa wanaoshikiliwa ni wanawake na watoto.
Shirika hilo la Haki za Binadamu limesema limetoa ushahidi wa madai ya uhalifu wa kivita kwa serikali ya Cameroon, lakini halikupata majibu yoyote.
Eneo la kaskazini mwa Cameroon na mataifa ya jirani kwa miaka kadhaa limekuwa likiharibiwa na mapigano yanayoendelea kati ya majeshi ya usalama na wapiganaji wa Boko Haramu.