Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Rais Magufuli awaonya wanaotaka kuvunja muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli ametoa tahadhari kwa yeyote yule atakayejaribu kuvunja muungano uliopo kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Onyo hilo amelitoa leo mjini Dodoma wakati wa maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, yaliyofanyika mjini Dodoma.
Aidha Rais Magufuli amekiri kuwa licha ya mafanikio yaliyopatikana bado kuna changamoto mbalimbali zinazoukabili Muungano huo.