Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mahakama yakataa kurejesha marufuku ya Trump
Mahakama ya Rufaa nchini Marekani imekataa kuirudisha tena marufuku iliyowekwa na Rais wa Marekani Donald Trump ya wasafiri kutoka nchi saba za kiislamu na Wakimbizi wote kuingia nchini Marekani.
Jopo la majaji watatu limepinga kwa kauli moja kubadilisha uamuzi uliotolewa na jaji wa jimbo la Washington ambaye wiki iliyopita alizuwia sehemu ya amri iliyotolewa na rais.
Bwana Trump amesema kuwa ulikuwa ni uamuzi wa kisiasa na hatimaye itapitishwa.